Swahili
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya count 26
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ
( 1 ) 
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ خَاشِعَةٌ
( 2 ) 
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٌ نَّاصِبَةٌ
( 3 ) 
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصْلَىٰ نَارًا حَامِيَةً
( 4 ) 
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسْقَىٰ مِنْ عَيْنٍ آنِيَةٍ
( 5 ) 
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيْسَ لَهُمْ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٍ
( 6 ) 
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسْمِنُ وَلَا يُغْنِي مِن جُوعٍ
( 7 ) 
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاعِمَةٌ
( 8 ) 
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعْيِهَا رَاضِيَةٌ
( 9 ) 
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٍ
( 10 ) 
Katika Bustani ya juu.
لَّا تَسْمَعُ فِيهَا لَاغِيَةً
( 11 ) 
Hawatasikia humo upuuzi.
فِيهَا عَيْنٌ جَارِيَةٌ
( 12 ) 
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٌ مَّرْفُوعَةٌ
( 13 ) 
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكْوَابٌ مَّوْضُوعَةٌ
( 14 ) 
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصْفُوفَةٌ
( 15 ) 
Na matakia safu safu,
وَزَرَابِيُّ مَبْثُوثَةٌ
( 16 ) 
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ
( 17 ) 
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ
( 18 ) 
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ
( 19 ) 
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ
( 20 ) 
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ
( 21 ) 
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسْتَ عَلَيْهِم بِمُصَيْطِرٍ
( 22 ) 
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
( 23 ) 
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ اللَّهُ الْعَذَابَ الْأَكْبَرَ
( 24 ) 
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيْنَا إِيَابَهُمْ
( 25 ) 
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا حِسَابَهُم
( 26 ) 
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!